UFANYE NINI UKIWA UNAPATA MAUMIVU KWENYE KUNYONYESHA FAHAMU

 Ufanye nini unapopata maumivu ya maziwa wakati wa  kunyonyesha?


Mara kadhaa wanawake wanaonyonyesha hupata maumivu ya maziwa. Hali hiyo inaambatana na ziwa kuvimba na kuwa jekundu. Tatizo hilo husababishwa na kuziba kwa mirija midogo inayosafirisha maziwa kupeleka kwenye chuchu. Maambukizi ya bakteria hufuatia baada ya mirija kuziba.


Dalili


•Kuhisi maumivu kama ziwa  linawaka moto 


•Ziwa kuvimba na kuwa na ugumu


•Kupata maumivu wakati wa kunyonyesha


•Wakati mwingine mama anapata  homa, 


Matibabu


Iwapo mama amepata tatizo hili anahitaji kufanya mambo yafuatayo kama sehemu ya matibabu


•Pata muda wa kutosha kupumzika. 


•Tumia vinywaji au vyakula vyenye majimaji kwa wingi


•Nyonyesha mtoto mara nyingi uwezavyo mfano kila baada ya saa 2-3. Mama anaponyonyesha itamsaidia kuondoa maambukizi na pia ni salama kwa mtoto. Mdomo wa mtoto unapaswa kufunguka sana, na chuchu yote  ingizwe ndani ya mdomo wa mtoto.


•Anza kunyonyesha upande wenye maumivu, ili mtoto aweze kumaliza maziwa yote kabla hajashiba.


•Kanda ziwa taratibu  kwa kutumia kitambaa safi na maji ya vuguvugu.




•Iwapo mama anapata homa anahitaji kutumia dawa 

0684450076


#Share na marafiki wajifunze pia


watsapp

watsapp

Comments

Popular posts from this blog

FAHAMU SIRI ZA DAWA ZA VIDONDA VYA TUMBO

NMN KUTIBU SUKARI,PRESHA,TEZI DUME NA NI ANT_AGING

JINSI YA KUPIKA MBOGA ZA MAJANI KUPATA VIRUTUBISHI VYAKE NA FAIDA ZAKE