Faida Za mboga za Majani

 :Mboga za Majani huwa na Nyuzinyuzi zinazosaidia kuboresha Mfumo wa Chakula na kutoa Kinga dhidi ya #Saratani ya Utumbo Mkubwa


Pia, huwa na Madini ya Potassium ambayo husaidia kudhibiti Shinikizo Kubwa la Damu na Magonjwa ya Moyo


Soma zaidi nakala za hivi



Hakuna aina moja ya mboga za majani inayotosha kukupatia virutubisho vyote muhimu ili uweze kuimarisha afya yako.


Ni muhimu kutokutumia aina moja ya mboga kila siku kwa kuwa haiwezi kukupatia virutubisho vyote unavyohitaji, bali jitahidi kuchanganya au kubadili mara kwa mara ili uweze kunufaika vizuri.


Mboga za majani huwa na faida zifuatazo kwa afya-

Huwa na nyuzinyuzi zinazosaidia kuboresha mfumo wa chakula, kurahisisha choo na kutoa kinga dhidi ya saratani ya utumbo mkubwa

Aina nyingi za mboga za majani huwa na madini ya potassium ambayo husaidia kudhibiti shinikizo kubwa la damu na magonjwa ya moyo

Huwa na kipimo kidogo cha sukari (Low Glycemic Index) hivyo hufaa sana kwa watu wenye tatizo la ugonjwa wa kisukari

Kama ilivyo kwa makundi mengine ya chakula, mboga za majani hubeba virutubisho muhimu kwa afya yako kama vile vitamini A, vitamini C, asidi ya foliki, madini mbalimbali na viondoa sumu. Vyote hivi huhitajika mwilini ili kujenga afya.

Comments

Popular posts from this blog

FAHAMU SIRI ZA DAWA ZA VIDONDA VYA TUMBO

NMN KUTIBU SUKARI,PRESHA,TEZI DUME NA NI ANT_AGING

JINSI YA KUPIKA MBOGA ZA MAJANI KUPATA VIRUTUBISHI VYAKE NA FAIDA ZAKE