:Mboga za Majani huwa na Nyuzinyuzi zinazosaidia kuboresha Mfumo wa Chakula na kutoa Kinga dhidi ya #Saratani ya Utumbo Mkubwa Pia, huwa na Madini ya Potassium ambayo husaidia kudhibiti Shinikizo Kubwa la Damu na Magonjwa ya Moyo Soma zaidi nakala za hivi Hakuna aina moja ya mboga za majani inayotosha kukupatia virutubisho vyote muhimu ili uweze kuimarisha afya yako. Ni muhimu kutokutumia aina moja ya mboga kila siku kwa kuwa haiwezi kukupatia virutubisho vyote unavyohitaji, bali jitahidi kuchanganya au kubadili mara kwa mara ili uweze kunufaika vizuri. Mboga za majani huwa na faida zifuatazo kwa afya- Huwa na nyuzinyuzi zinazosaidia kuboresha mfumo wa chakula, kurahisisha choo na kutoa kinga dhidi ya saratani ya utumbo mkubwa Aina nyingi za mboga za majani huwa na madini ya potassium ambayo husaidia kudhibiti shinikizo kubwa la damu na magonjwa ya moyo Huwa na kipimo kidogo cha sukari (Low Glycemic Index) hivyo hufaa sana kwa watu wenye tatizo la ugonjwa wa kisukari Kama ilivyo k...
FAHAMU:NAMNA YA KUPIKA MBOGA ZA MAJANI Watu wanakula mboga za majani kwa lengo la kupata kiburudisho na wengine ili siku iende tuu. Wengi wanakosea kupika mboga za majani ili kupata virutubisho kama vitamins na madini chuma Zingatia haya ukiwa unapika mboga 1.Osha mboga za majani kwa maji safi kabla ya kuzikatakata. Kamwe usioshe baada ya kuzikatakata 2. Pika kwa muda mchache. Virutubisho vyake ni heat labile; ukichemsha sana vinaharibika. 3. Pika ukiwa umefunika kwa mfuniko. Kuacha wazi kutapoteza virutubisho 4. Usipike chukuchuku (bila mafuta); virutubisho vinavyopatikana kwenye mbogamboga vinahitaji kiasi cha mafuta ili kimeng'enywe na kuingia kwenye mfumo wa damu wa mlaji. Hivyo, ukila bila kuweka mafuta, unapoteza virutubisho vingi. Weka mafuta salama kwa mlaji hata kijiko kimoja tu. Gusa hapa chati nami Watsapp FAIDA ZA KULA MBOGA ZA MAJANI 1. Kupata virutubisho muhimu kama vitamins ili kusaidia kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili na mfumo wa fa...
Comments
Post a Comment